Friday, July 28, 2017

ROMA BADO HAWAJAKATA TAMAA KWA MAHREZ.

KLABU ya AS Roma inajipanga kutoa ofa mpya ya paund milioni 32 kwa ajili ya Riyad Mahrez ambaye ameendelea kluonyesha kiwango kikubwa katika mechi za maandalizi ya msimu mpya. Mahrez tayari ameshafunga mabao mawili kuelekea msimu mpya baada ya kuifungia Leicester City bao la ushindi kwenye mchezo wao dhidi ya Luton juzi usiku. Hilo linakuwa bao lake la pili mwezi huu baada ya pia kufunga kwenye mchezo dhidi ya West Bromwich Albion huko Asia. Lakini nyota huyo wa kimataifa wa Algeria anataka kuondoka Leicester baada ya kuwaambia mabingwa hao wa Ligi Kuu msimu wa 2015-2016 kuwa ataondoka msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment