Friday, July 28, 2017

THOMAS LEMAR ANUKIA ARSENAL.

KLABU ya Arsenal inadaiwa kukaribia kunasa saini ya nyota wa AS Monaco Thomas Lemar kwa kitita cha paundi milioni 45. Arsenal wamekuwa wakihangaika kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa na taarifa zinadai kuwa hatimaye wamefanikiwa kufikia makubaliano. Tayari ofa kadhaa za Arsenal kwa ajili ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 21 zimekataliwa na Monaco ambao wenyewe wanataka paundi milioni 80 kwa mchezaji huyo waliyemsajili kutoka Caen miaka miwili iliyopita. Taarifa kutoka Uingereza zinadai kuwa mapema mwezi huu kuwa Lemar alishafikia makubaliano na Arsenal na kuwahabalisha mabingwa hao wa Ufaransa kuwa anataka kuondoka.

No comments:

Post a Comment