Friday, July 28, 2017

LACAZETTE KUCHEZA KWA MARA YA KWANZA MBELE YA MASHABIKI WA EMIRATES.

MSHAMBULIAJI mpya wa Arsenal, Alexandre Lacazette anatarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza mbele ya mashabiki wa nyumbani mwishoni mwa wiki hii katika mechi ya Kombe la Emirates. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger aliweka rekodi ya klabu kwa kutoa kitita cha paundi milioni 52 kumsajili Lacazette kutoka Olympique Lyon na mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa anatarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza Uwanja wa Emirates wakati klabu hiyo itakapocheza na Benfica Jumamosi hii. Michuano hiyo ya kirafiki inayoshirikisha timu nne ni muhimu kwa Lacazette kujiweka fiti kabla ya Arsenal haijaanza kampeni zake za Ligi Kuu kwa kucheza na Leicester City Agosti 11 baada ya kuwa tayari wamecheza mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya Chelsea wiki ijayo. Akizungumza na wanahabari, Lacazette amesema Arsenal ni klabu kongwe na katika kipindi chote cha utotoni amekuwa na ndoto ya kuichezea kutokana na nyota kadhaa wa Ufaransa waliowahi kupitia hapo akiwemo Thierry Henry.

No comments:

Post a Comment