Friday, July 28, 2017

WEST HAM KUMKOSA ANTONIO MECHI DHIDI YA UNITED.

KIUNGO wa West Ham United, Michail Antonio bado ameendelea kujiuguza kufuatia kufanyiwa upasuaji wa msuli wa nyuma ya paja lakini anatarajiwa kukosa mechi ya ufunguzi wa Ligi Kuu dhidi ya Manchester United. Antonio ambaye alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa klabu msimu uliopita, amekuwa akijiuguza majeruhi hayo yaliyokatisha kampeni zake Aprili mwaka huu kwenye ushindi wa bao 1-0 waliopata dhidi ya Swansea Cioty. Antonio sambamba na mchezaji mwenzake Andy Carroll ambaye pia amekuwa nje kwa majeruhi ya kipindi kirefu, waliachwa kwenye kikosi cha timu hiyo ambacho kilifanya ziara ya maandalizi ya msimu mpya huko Austria na Ujerumani. Meneja wa klabu hiyo Tony Bilic alithibitisha taarifa hizo wakati akizungumza na wanahbari nchini Ujerumani na kuongeza kuwa Antonio atakosa mechi moja dhidi ya United.

No comments:

Post a Comment