Friday, July 28, 2017

GUARDIOLA ANATAKA KUENDELEA KUBAKI cITY KWA KIPINDI KIREFU ZAIDI.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola atakuwa tayari kuongeza mkataba mwingine kufuatia kutaka kuendelea kubakia kwa kipindi kirefu iwezekanavyo katika klabu hiyo. Guardiola alisaini mkataba wa miaka mitatu na City wakati alipoteuliwa kuchukua nafasi ya Manuel Pellegrini mwaka jana. Msimu wake wa kwanza Uingereza ulishuhudia kumaliza akiwa mikono mitupu bila taji lolote kwa mara ya kwanza toka aanze shughuli hiyo ya ukocha lakini usajili mkubwa unaofanywa na klabu hiyo hivi sasa una nia ya kusahihisha makosa kwenye msimu ujao wa 2017-2018. City imefanya usajili mkubwa katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi kwa kuwanasa nyota kadhaa akiwemo bernardo Silva, Kyle Walker, Danilo na Benjamin Mendy na Guardiola ana matumaini ya kukaa hapo kwa kipindi kirefu ili kuona mipango yake ikifanikiwa. Akizungumza na wanahabari, Guardiola amesema hafahamu litakalotokea huko mbele lakini angependa kuendelea kuinoa City kwa kipindi kirefu zaidi ili kuona inafanikiwa na kuendelea kukaa kwenye nafasi za juu.

No comments:

Post a Comment