Tuesday, July 18, 2017

LEICESTER HAIJAPATA OFA KWA MAHREZ - SHAKESPEARE.

MENEJA wa Leicester City, Craig Shakespeare amedai kuwa hawajapokea ofa yeyote kwa ajili ya Riyad Mahrez pamoja na winga huyo kuhusishwa na tetesi za kuwania na Arsenal na AS Roma. Mustakabali wa Mahrez bado haujajulikana toka Leicester watwae taji la Ligi Kuu msimu wa 2015-2016 ambapo nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 aliamua kubakia msimu uliopita ili aweze kuwa sehemu ya kikosi katika kampeni zao za Ligi ya Mabingwa Ulaya. Baada ya Leicester kumaliza katika nafasi ya 12 msimu wa 2016-2017, Mahrez alithibitisha nia yake ya kuondoka Uwanja wa King Power kwa kutoa taarifa hiyo Mei mwaka huu lakini mpaka sasa bado amebakia kuwa mchezaji wa Leicester. Roma wana matumaini ya kumsjaili nyota huyo wa kimataifa wa Algeria na kuna taarifa kuwa anaweza kukubali kwenda Italia kama Arsenal wasipomtafuta. Akizungumza na wanahabari, Shakespeare amesema anadhani Mahrez aliweka wazi msimu wake lakini mpaka sasa hakuna timu yeyote iliyotuma ofa rasmi hivyo ataendelea kuwa mchezaji wao.

No comments:

Post a Comment