Monday, July 17, 2017

DIEGO COSTA APIGA PICHA AKIWA NA JEZI YA ATLETICO.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Hispania, Diego Costa amepiga picha za video akifurahia likizo yake huku akiwa amevaa jezi ya Atletico Madrid. Katika picha hizo za video kwenye mtandao wake wa Instagram, nyota huyo alivaa jezi ya timu yake hiyo ya zamani, huku akiandika ujumbe kwa mchezaji mwenzake Cesc Fabregas kuwa amkumbatie meneja wao Antonio Conte. Mustakabali wa Costa bado haujawekwa sawa toka nyota huyo alipobainisha kuwa Conte alimwambia kuwa hahitajiki tena kwenye klabu hiyo. Matokeo hayo yamemfanya Costa mwenye umri wa miaka 28 kuachwa katika kikosi cha Chelsea kilichoanza maandalizi ya msimu mpya huku kukiwa na matumaini ya kupata klabu mpya.

No comments:

Post a Comment