Monday, July 17, 2017

HART KUFANYIWA VIPIMO VYA AFYA WEST HAM.

KIPA Joe Hart anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya katika klabu ya West Ham United ili kukamilisha uhamisho wake wa mkopo kutoka Manchester City. West Ham walikuwa wakitafuta kipa mpya kipindi hiki cha majira ya kiangazi na wamefanikiwa kumshawishi kipa huyo wa kimataifa wa Uingereza. Mkataba wa Hart unatarajiwa kumalizika mwaka 2019 katika klabu ya City na inadaiwa kuwa tayari alishaambiwa atafute klabu mpya na meneja Pep Guardiola. City walimruhusu Hart aende kwa mkopo katika klabu ya Torino msimu uliopita na sasa anatarajiwa kuhamia Uwanja wa London huku Guardiola akiwa tayari kumlipa nusu ya mshahara wake.

No comments:

Post a Comment