Monday, July 10, 2017

ROONEY ADOKEZA ZIARA YA TANZANIA.

MSHAMBULIAJI mpya wa Everton, Wayne Rooney amesema anasubiri kwa hamu ziara ya Tanzania akiwa na klabu hiyo. Rooney aliyerejea Everton baada ya kupita miaka 13, anatarajiwa kuwa kwenye kikosi cha timu hiyo ambacho kitatua Tanzania kwa ajili ya mechi moja ya kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya. Akizungumza na luninga ya klabu hiyo, Rooney amesema anaisubiri kwa hamu ziara hiyo ya kwenda Tanzania kani anadhani itakuwa safari nzuri itakayomuwezesha kufahamiana vyema na wenzake. Rooney aliendelea kuwa ziara kama hizo huwa nzuri kwani ni vizuri kukaa hotelini na wachezaji, kujumuika nao na kuwafahamu zaidi. Rooney amesema hajawahi kufika Tanzania hivyo ana hamu kubwa ya kutua katika taifa hilo la Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment