Monday, July 10, 2017

COSTA AACHWA KIKOSI CHA CHELSEA KINACHOANZA ZIARA YA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Hispania, Diego Costa hajajiunga na kikosi cha Chelsea kwa ajili ya mazoezi ya maandalizi ya msimu mpya baada ya kupewa ruhusa ili aweze kukamilisha uhamisho wake kwenda Atletico Madrid. Atletico ndio imebaki chaguo pekee kwa Costa ambaye tayari alishahabalishwa na meneja Antonio Conte kwa njia ya ujumbe kuwa hahitajiki Stamford Bridge mwezi uliopita. Chelsea na Atletico tayari zimeanza mazungumzo lakini hawajafikia muafaka kuhusu ada na Costa anaonekana yuko radhi kukubali chochote atakachoambiwa na klabu yake hiyo ya zamani. Kufuatia kushindwa na Manchester United katika mbio za kumuwania Romelu Lukaku, Chelsea watalazimika kuingia sokoni tena kutafuta mbadala wa Costa kabla ya kuanza kwa msimu ujao wa Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment