Monday, July 10, 2017

LUKAKU AAGA RASMI EVERTON.

MSHAMBULIAJI Romelu Lukaku ametuma ujumbe wa kuaga kwa klabu ya Everton wakati akijiandaa kukamilisha usajili wake kwenda Manchester United. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 alifanyiwa vipimo vya afya mwishoni mwa wiki iliyopita na anatarajiwa kusajili na United kwa kitita cha paundi milioni 75, pamoja na klabu yake ya zamani ya Chelsea nayo kufikia kiwango hicho. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji akitua Everton akitokea Chelsea kwa kitita cha paundi milioni 28 Julai mwaka 2014 na ameshafunga mabao 68 katika Ligi Kuu. Lukaku alituma ujumbe katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram akiwashukuru watu wote waliofanya kazi pamoja Everton. Lukaku pia aliwashakuru mashabiki kwa kumuunga kwa muda wote wa miaka minne aliyokuwa nao pamoja na ni heshima kubwa kucheza mbele yao.

No comments:

Post a Comment