Thursday, July 6, 2017

RB LEIPZIG YAIBANIA LIVERPOOL KWA KEITA.

KLABU ya Liverpool imepata pigo lingine katika jitihada zao za kuwania kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita kufuatia klabu hiyo ya Bundesliga kuzizitiza hatamuuza kwa bei yeyote ile. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 22, anawindwa kwa udi na uvumba na meneja Jurgen Klopp baada ya kuisaidia Ujerumani kumaliza katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi msimu uliopita juu ya Borussia Dortmund lakini wakiachwa kwa mbali kidogo na Bayern Munich. Taarifa zilikuwa zinadai Liverpool walihitajika kuvunja rekodi ya usajili Bundesliha kwa kutoa paundi milioni 66 katika mbio zao za kumuwania Keita lakini sasa ndoto hizo zinaonekana kuyeyuka. Akizungumza na wanahabari kuhusiana na suala hilo, afisa usajili wa Leipzig, Ralf Rangnick amesema hawana mpango wowote wa kuachia wachezaji wao muhimu kuondoka kipindi hiki. Liverpool wanataka kuongeza kiungo wa kati, beki wa kushoto na beki wa kati kabla ya kuanza kwa msimu wa Ligi Kuu baada ya kuwa tayari wameshawasajili winga Mohamed Salah kutoka AS Roma na mshambuliaji Dominic Solanke kutoka Chelsea.

No comments:

Post a Comment