Thursday, July 6, 2017

TANZANIA YAKWEA VIWANGO FIFA.

TANZANIA imekwea kwa nafasi 25 katika viwango vya ubora duniani vinavyotolewa kila mwezi na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA. Katika viwango vilivyopita ambavyo vilitolewa Juni mosi Tanzania ilishuka kwa nafasi nne mpaka nafasi ya 139 lakini kwenye viwango vipya vilivyotolewa mapema leo imekwea mpaka nafasi ya 114. Mbali na kukwea viwango hivyo duniani lakini pia kwa upande wa Afrika Mashariki nako wamepanda mpaka nafasi ya tatu baada ya kushika nafasi ya 30 kwa upande wa Afrika wakizidiwa na Uganda waliopo nafasi ya 74 duniani na 15 Afrika na Kenya waliopo nafasi ya 84 duniani na 18 Afrika. Nchi zingine za Afrika Mashariki ni Burundi waliopo nafasi 121 duniani na 35 kwa Afrika, Rwanda nafasi ya 127 duniani na 36 na Sudan Kusini ndio wa mwisho wakishika nafasi ya 143 duniani na 43 Afrika. Kwa upande wa Orodha za Afrika Misri ndio kinara akishika nafasi ya 24 duniani akifuatiwa na Senegal waliopo nafasi ya 27, jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC nafasi ya 28, Tunisia nafasi ya 34 na wa tano ni mabingwa wa Afrika Cameroon waliopo nafasi ya 36. Katika orodha za jumla mabingwa wa dunia na Kombe la Shirikisho Ujerumani wamerejea kileleni wakifuatiwa na Brazil katika nafasi ya pili, Argentina nafasi ya tatu, Ureno nafasi ya nne na Switzerland nafasi ya tano.

No comments:

Post a Comment