Thursday, July 6, 2017

WENGER AELEZA SABABU ZA KUVUNJA BENKI KWA LACAZETTE.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amebainisha kitu alichokiona kwa Alexandre Lacazette na kwanini ana uhakika nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa ataweza kuisaidia timu hiyo kushindana katika kiwango cha juu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 amesajiliwa Arsenal akitokea Olympique Lyon kwa mkataba wa miaka mitano huku ada ya paundi milioni 52 ikiweka rekodi mpya na kuizidi ile ya Mesut Ozil aliyosajiliwa kwa kitita cha paundi milioni 42.5 kutoka Real Madrid mwaka 2013. Lacazette pia anatarajiwa kulipwa kitita cha paundi 200,000 kwa wiki, kiasi cha ambacho kitamfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi Emirates. Wenger amesema amefurahishwa na nyota huyo kujiunga nao kwani kwa miaka mingi ameonyesha anaweza kufunga mabao na ni mshambuliaji mwenye ufanisi wa hali ya juu, sambamba na ufundi na tabia njema.

No comments:

Post a Comment