Thursday, July 6, 2017

MAN UNITED YAKUBALI KUTOA PAUNDI MILIONI 75 KWA LUKAKU.

KLABU ya Manchester United inadaiwa kukubali kutoa kiasi kinachofikia paundi milioni 75 kwa ajili ya mshambuliaji wa Everton Romelu Lukaku. Nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 24 amefunga mabao 25 katika Ligi Kuu msimu uliopita. United ambao wamekuwa wakimfukuzia Lukaku zaidi kipindi hiki cha kiangazi, sasa hawadhaniwi kama watamuwania tena mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata. Uhamisho huo wa Lukaku hauhusiani na mazungumzo yaliyofanywa na mshauri wa Wayne Rooney pamoja na mwenyekiti wa Everton juu ya uwezekano wa nyota huyo kurejea tena katika timu hiyo. Meneja wa United, Jose Mourinho ana matumaini dili hilo litakalimika kwa wakati ili aweze kumjumuisha Lukaku katika kikosi chake kabla ya kuanza ziara ya maandalizi ya msimu mpya huko Marekani Jumapili hii.

No comments:

Post a Comment