Thursday, July 6, 2017

BARCELONA WATOSWA KWA PAULINHO.

KLABU ya Barcelona imekataliwa ofa yao ya paundi milioni 20 kwa ajili ya kumuwania kiungo wa zamani wa Manchester City, Paulinho ambaye kwasasa anakipiga katika timu ya Guangzhou Evergrande. Klabu hiyo ya China imetoa taarifa mapema leo kuwa Barcelona walituma ofa yao rasmi kwa ajili ya nyota huyo wa kimataifa wa Brazil lakini wamekataa kwakuwa hawana mpango wa kumuuza. Taarifa hiyo ilidai kuwa Paulinho tayari alishaongeza mkataba Januari mwaka huu na ni mchezaji muhimu katika kikosi chao kwasasa hivyo hawawezi kumuacha. Klabu hiyo pia imetoa shukrani kwa Barcelona ambao wameonyesha kumuhusudu sana Paulinho.

No comments:

Post a Comment