Thursday, July 6, 2017

RUDIGER AELEZA MAHABA YAKE KWA ARSENAL.

BEKI wa kimataifa wa Ujerumani, Antonio Rudiger anaweza kujiingiza katika bifu zito na mashabiki wa Chelsea kufuatia kauli yake aliyotoa kabla ya kujiunga na mabingwa hao wa Uingereza. Rudiger amekubali kujiunga na Chelsea na kwasasa inadaiwa tayari yuko jijini London kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kukamilisha usajili huo unaodaiwa kufikia paundi milioni 36. Lakini pamoja na kwenda Chelsea, nyota huyo amekiri hadharani kuwa anaihusudu sana Arsenal na amekuwa akiifuatilia kwa kipindi kirefu. Rudiger amesema amekuwa akiifuatilia Arsenal toka enzi za kina Thierry Henry na Dennis Bergkamp na kwamba moyo wake unaipenda klabu hiyo. Beki huyo anatarajia kupewa mkataba wa miaka mitano na Chelsea.

No comments:

Post a Comment