Wednesday, July 5, 2017

TORRES AONGEZA MWAKA MMOJA ATLETICO.

MSHAMBULIAJI wa Atletico Madrid, Fernando Torres amesaini mkataba wa mwaka mmoja ambao utamuweka katika klabu hiyo mpaka Juni mwaka 2018. Akizungumza na tovuti ya klabu hiyo mara baada ya kusaini mkataba huo, Torres amesema amefurahishwa kuendelea kubakia hapo kwa mwaka mmoja zaidi. Baada ya kuibuka katika kikosi cha kwanza cha Atletico mwaka 2001, mshambuliaji huyo aliimarika na kuwa nahodha kabla ya kujiunga na Liverpool mwaka 2007. Torres ambaye ametwaa mataji mwili ya Ulaya na moja la Kombe la Dunia akiwa na Hispania, pia amecheza kwa vipindi vifupi Chelsea na AC Milan kabla ya kurejea Atletico mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment