Wednesday, July 5, 2017

LACAZETTE ASAINI MIAKA MITANO ARSENAL.

KLABU ya Arsenal imefanikiwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Alexandre Lacazette kutoka Olympique Lyon kwa kitita kilichovunja rekodi ya klabu cha paundi milioni 46.5 na kupewa mkataba wa miaka mitano. Ada hiyo ambayo inaweza kufikia hadi paundi milioni 52.6 ukijumlisha na nyongeza nyingine, itaipita ile ya paundi milioni 42.4 Arsenal waliyolipa Real Madrid kwa ajili ya Mesut Ozil mwaka 2013. Akizungumza na wanahabari, Lacazette amesema Arsenal ni klabu inayocheza soka la kupendeza nchini Uingereza hivyo alihitaji sana kuja kuichezea. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 anatarajiwa kusafiri na kikosi cha timu hiyo mwishoni mwa wiki hii kwa ajili ya mechi mbili za kirafiki jijini Sydney wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment