Wednesday, July 5, 2017

MADRID YAVUNJA MWIKO WA MIAKA 17 KWA KUNASA KINDA KUTOKA ATLETICO.

KLABU ya Real Madrid imefanikiwa kumsajili beki wa kushoto Theo Hermandez kutoka kwa mahasimu wao wa jiji Atletico Madrid na kumpa mkataba wa miaka sita. Hernandez anakuwa mchezaji wa kwanza katika kipindi cha miaka 17 kusajiliwa moja kwa moja kutoka Atletico baada ya kiungo wa kimataifa wa Argentina, Santiago Solari kufanya hivyo mwaka 2000. Chipukizi huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 19 alishindwa katika kikosi cha kwanza cha Atletico na kuutumia msimu uliopita kwa mkopo kwenye kikosi cha Alaves. Akiwa Alaves amecheza mechi 38 za mashindano yote ikiwemo fainali ya Kombe la Mfalme ambapo walifungwa na Barcelona. 
Katika hatua nyingine beki Fabio Coentrao amejiunga na klabu ya Sporting Lisbon ya Ureno kwa mkopo wa mwaka mmoja. Coentrao alijiunga na Madrid akitokea kwa mahasimu wa Sporting, Benfica kwa kitita cha paundi milioni 27 mwaka 2011 na kufanikiwa kushinda taji moja la La Liga na mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment