Tuesday, July 4, 2017

MONCHENGLADBACH YANASA BEKI WA DORTMUND.

KLABU ya Borussia Monchengladbach imefanikiwa kumsajili beki wa kimataifa wa Ujerumani Matthias Ginter kutoka Borussia Dortmund kwa kitita cha euro milioni 17. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 amesaini mkataba unaomalizika mwaka 2021 kuitumikia klabu hiyo. Ginter alikuwa sehemu ya kikosi cha Ujerumani kilichoitandika Chile bao 1-0 Jumapili iliyopita na kutwaa taji la michuano ya Kombe la Shirikisho. Mkurugenzi wa michezo wa Dortmund, Michael Zorc amesema Ginter alimueleza nia yake ya kuondoka kwasababu ya ushindani wa nafasi uliopo kwenye kikosi cha timu hiyo.

No comments:

Post a Comment