Tuesday, July 4, 2017

MWAMUZI ASHAMBULIWA KUFUATIA KUTOA PENATI YENYE UTATA.

CHAMA cha soka cha China-CFA kimethibitisha kuwa kundi la watu 10 limewashambulia waamuzi kufuatia sare yenye utata iliyopatikana katika mchezo wa Ligi Daraja la Pili nchini humo. Mwamuzi wa kati na wasaidizi wake walishambuliwa katika vyumba vya hoteli waliyofikia muda mfupi baada ya umeme kukatwa. Taarifa ya CFA imedai kuwa waamuzi hao waliachwa na majeraha ya kichwani, kiuno na miguu na tayari polisi wameanza uchunguzi wa tukio hilo. Tukio hilo limetokea kufuatia mchezo uliomalizika kwa utata kati ya Baoding Rongda na Wuhan Zall ambao ulicheza Jumamosi iliyopita.

No comments:

Post a Comment