Tuesday, July 4, 2017

MOURINHO ACHUKIZWA NA USJAILI WA UNITED.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amedaiwa kutofurahishwa na taratibu za klabu hiyo katika usajili wa kipindi hiki cha kiangazi. Baada ya United kutwaa taji la michuano ya Europa League Mei 24 mwaka huu, Mourinho amesema alimpa makamu mwenyekiti Ed Woodward orodha na wachezaji anawahitaji katika usajili. Taarifa za ndani zinadai kuwa orodha hiyo ilikuwa na mahitaji machache ya wachezaji watatu au wanne pekee. Kuna uwezekano kukawa na maendeleo mengine wiki hii lakini mpaka sasa ni mchezaji mmoja mpya aliyesajili ambaye ni beki wa Benfica, Victor Lindelof aliyetua Old Trafford kwa kitita cha paundi milioni 31. Inaaminika kuwa Mourinho anataka angalau mshambuliaji mmoja ili kuziba nafasi ya Zlatan Ibrahimovic pamoja na mchezaji wa nafasi ya kiungo wa ulinzi.

No comments:

Post a Comment