Tuesday, July 4, 2017

ARSENAL YASUBIRI VIPIMO KUKAMILISHA USAJILI WA LACAZETTE.

KLABU ya Arsenal inadaiwa kujipanga kumtangaza Alexandre Lacazette kuwa mchezaji wao mpya baada ya kufikia makubaliano ya kumsajili na Olympique Lyon. Arsenal wamekuwa wakimfukuzia mshambuliaji huyo kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita na walikataliwa mara mbili na Lyon katika kipindi cha usajili wa majira ya kiangazi mwaka jana. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anadaiwa kwenda nchini Ufaransa mwezi uliopita lakini alikataliwa tena kabla ya taarifa ya makubaliano kutolewa wiki iliyopita. Taarifa kutoka nchini Ufaransa zinadai kuwa Lacazette sasa anaweza kusaini mkataba huo na Arsenal wakati wowote kutokea sasa.

No comments:

Post a Comment