Tuesday, July 4, 2017

KOREA KUSINI WAPATA KOCHA MPYA.

CHAMA cha Soka cha Korea Kusini, kimemteua Shin Tae-yong kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya nchi hiyo. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 46 ambaye enzi zake alikuwa akicheza nafasi ya kiungo, anachukua nafasi ya Uli Stielike wa Ujerumani aliyetimuliwa mwezi uliopita kufuatia kupata matokeo mabaya ambayo yamefanya kuhatarisha nafasi ya Korea Kusini kufuzu michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Shin ambaye amepewa mkataba wa mwaka mmoja, aliichezea kwa misimu 12 klabu ya Ilhwa Chunma ya nchi hiyo huku pia akicheza mechi 13 katika kikosi cha timu ya taifa. Shin amekuwa sehemu ya benchi la ufundi la kikosi cha timu ya taifa ya vijana ya nchi hiyo toka mwaka 2015 na alikiongoza kikosi cha vijana chini ya umri wa miaka 20 kutinga hatua ya mtoano ya 16 kwenye michuano ya Kombe la Dunia iliyofayika kwenye ardhi yao mapema mwaka huu.

No comments:

Post a Comment