Thursday, July 20, 2017

MOURINHO ALIA NA USAJILI MGUMU.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amesema anaweza kufanya usajili wa mchezaji mmoja zaidi kwasababu ya ugumu wa dirisha la usajili kipindi hiki cha majira ya kiangazi. Mourinho amedai kuwa klabu nyingi zinahitaji kiasi walichoweka kwa ajili ya wachezaji. Akizungumza na wanahabari kuhusiana na suala hilo, Mourinho ambaye ameshasajili wachezaji wawili kati ya wanne aliohitaji amesema United sio klabu iliyoko tayari kulipa kiasi ambacho klabu zinataka. Mourinho aliendelea kudai kuwa amezoea klabu zinazotoa fedha nyingi kwa wachezaji wakubwa, sasa kila mtu analipa fedha nyingine kwa mchezaji mzuri. United imetumia kitita cha paundi milioni 75 kwa ajili ya mshambuliaji wa Everton Romelu Lukaku na kiasi cha paundi milioni 31 kwa ajili ya beki wa Benfica Victor Lindelof.

No comments:

Post a Comment