Tuesday, July 18, 2017

POLISI WAMSHIKILIA "MALINZI" WA HISPANIA KWA TUHUMA ZA UBADHILIFU.

POLISI nchini Hispania imedai kumshikilia rais wa Shirikisho la Soka la Hispania na mtoto wake wa kiume ikiwa ni sehemu ya uchunguzi wa masuala ya rushwa. Rais huyo Angel Maria Villar Llona mwenye umri wa miaka 67 alikamatwa kwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha. Villar ambaye amewahi kuwa mchezaji wa zamani wa nchi hiyo, amekuwa rais wa shirikisho hilo toka mwaka 1988. Mwanaye Gorka pia ni miongoni mwa watu kadhaa wengine waliokamatwa wakati wa msako huo uliofanyika mapema leo.

No comments:

Post a Comment