Tuesday, July 18, 2017

STARS YAIFUATA MAPEMA AMAVUBI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Salum Mayanga ametangaza mabadiliko kidogo katika mipango yake ya kujiandaa na mchezo wa marudiano dhidi Rwanda unaotarajiwa kufanyika Jumamosi hii. Awali Stars walikuwa wafanye mazoezi kwa muda wa siku tatu jijini Mwanza yaani Jumatatu, Jumanne na Jumatano kabla ya kuanza kufunga safari kuelekea jijini Kigali kwa ajili ya mchezo wao huo. Akizungumza na wanahabari mapema leo, Ofisa habari wa Shirikisho la Soka nchini-TFF, Alfred Lucas amesema Stars sasa haitafanya tena mazoezi kesho na badala yake watasafiri kurejea jijini Dar es Salaam na kuunganisha moja kwa moja mpaka Kigali. Lucas amesema sababu kubwa na kocha Mayanga kufanya hivyo ni kutoa nafasi zaidi kwa kikosi cha Stars kuzoea mazingira na hali ya hewa ya huko kabla ya mchezo wao huo muhimu wa kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani-CHAN. Kwenye mchezo wa kwanza Stars walitoka sare ya ya bao 1-1 dhidi ya Rwanda na sasa wanahitaji ushindi wa aina yeyote au sare ya mabao kuanzia 2-2 ili waweze kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kufuzu michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment