Monday, August 21, 2017

ARSENAL HUENDA IKAMUUZA MUSTAFI

KLABU ya Arsenal inadaiwa kukataa ya mkopo kutoka Inter Milan kwa ajili ya beki wake wa kimataifa wa Ujerumani Shkodran Mustafi wiki iliyopita. Hata hivyo taarifa zinadai kuwa Arsenal wanaweza kukubali kumuuza beki huyo kama Inter wataweza kutoa kiasi cha milioni 35 ambacho walilipa wakati walimnyakuwa kutoka Valencia kiangazi mwaka jana. Mustafi amekuwa akipata kwenye kikosi cha kwanza cha Arsenal lakini amekuwa akipata tabu kidogo kuelewana na wachezaji wenzake hatua ambayo inaweza kupelekea suala la kuuzwa liwezekane. Kama Arsenal ikiamua kumuuza nyota huyo mwenye umri wa miaka 25, italazimika kutafuta mbadala wake ili kuimarisha safu yao ya ulinzi.

No comments:

Post a Comment