Monday, August 21, 2017

WEST BROM WAIKATIA RUFANI KADI NYEKUNDU YA ROBSON-KANU

KLABU ya West Bromwich Albion imekata rufani dhidi ya kadi nyekundu aliyoonyeshwa Hal Robson-Kanu katika ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Burnley kwenye mchezo wa Ligi Kuu jana. Mshambuliaji huyo alitolewa nje dakika za mwishoni kufuatia kumchezea hovyo beki wa Burnley Matthew Lowton. Robson-Kanu ndiye aliyefunga bao pekee kwenye mchezo huo na kuifanya West Brom kuanza vyema mechi zao mbili za mwanzo za ligi. Taarifa ya West Brom imedai kuwa watatuma malalamiko yao kutokana na uamuzi huo kwenda Shirikisho la Soka la Uingereza-FA.

No comments:

Post a Comment