Monday, August 21, 2017

NEYMAR AWASHAMBULIA VIONGOZI WA BARCELONA

MSHAMBULIAJI wa Paris Saint-Germain-PSG, Neymar amewaponda wakurugenzi wa klabu yake ya zamani na kudai kuwa Barcelona inastahili viongozi bora zaidi yao. Akizungumza na wanahabari mara baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 6-2 waliopata PSG dhidi ya Toulouse, Neymar amesema viongozi wa Barcelona waliopo madarakani hawastahili kuwepo hapo. Neymar aliandelea kudai kuwa amekaa Barcelona kwa miaka minne na amekuwa na furaha wakati wote lakini sio kwa viongozi wa klabu hiyo. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil amesema Barcelona inastahili uongozi bora zaidi na dunia nzima inafahamu hilo.

No comments:

Post a Comment