Friday, August 25, 2017

DORTMUND YAKANUSHA KUMALIZANA NA BARCELONA

KLABU ya Borussia Dortmund imedai mapema leo kuwa hakuna makubaliano yeyote yaliyofikiwa kwa ajili ya uhamisho wa Ousmane Dembele kwenda Barcelona. Kauli hiyo ya Dortmund inakuja kufuatia taarifa kutoka nchini Ujerumani kudai kuwa tayari makubaliano baina ya pande hizo kwa ajili ya Dembele yamekamilika. Akizungumza na wanahabari, msemaji wa Dortmund amesema wamewapa muda Barcelona hivyo kuna kitu kinaweza kikatokea au kisitokee pia. Taarifa zingine zinadai kuwa Barcelona imekubali kutoa kitita cha euro milioni 120 hivuo kumfanya kuwa mchezaji wa pili ghali zaidi duniani baada ya Neymar.

No comments:

Post a Comment