Friday, August 25, 2017

LIVERPOOL YAMNYATIA SANCHEZ

KLABU ya Liverpool inadaiwa kujiandaa kumuwania kiungo wa Bayern Munich Renato Sanchez. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno ambaye alitua Allianz Arena majira ya kiangazi mwaka jana, anataka kutafuta timu atakayopata nafasi ya kucheza mara kwa mara na meneja Jurgen Klopp yuko tayari kufanikisha suala hilo. Sanchez ambaye alijizolea umaarufu mkubwa kutokana na kiwnago bora alichoonyesha katika michuano ya Ulaya akiwa na kikosi cha ushindi cha Ureno kiangazi mwaka jana, kwa kipindi kirefu amekuwa akihusishwa na tetesi za kuwaniwa na Manchester United. Bayern wanaweza kukubali kumuacha kwa mkopo kiungo huyo kwani bado wanamuhitaji nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 kwa siku zijazo.

No comments:

Post a Comment