Friday, September 1, 2017

PALACE YAMCHUKUA SAKHO MOJA KWA MOJA

KLABU ya Crystal Palace imefanikiwa kumsajili beki wa kati Mamadou Sakho kutoka Liverpool kwa kitita cha paundi milioni 26. Ofa hiyo ilikuwa ya nne kwa Palace kwa ajili ya kumuwania beki huyo mwenye umri wa miaka 27 baada ya Jumanne kukataliwa ofa yao ya paundi milioni 25. Liverpool walieleza kuwa hawatakubali kuchukua ofa chini ya paundi milioni 30 kwa ajili ya nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa ambaye alicheza kwa mkopo Selhurst Park msimu uliopita. Akizungumza na wanahabari mara baada ya kumalika kwa usajili huo, Sakho amesema anapenda changamoto aliyopata msimu uliopita, ilikuwa vigumu lakini ilimvutia ndio maana akaona sehemu sahihi ya kwenda ni Palace kipindi hiki cha kiangazi.

No comments:

Post a Comment