Thursday, August 2, 2012
SUAREZ AWAPONDA MASHABIKI WANAOMZOMEA.
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uruguay, Luis Suarez amewaponda mashabiki ambao walikuwa wakimzomea wakati timu yake ilipokubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Uingereza katika michuano ya Olimpiki akidai kuwa ni dalili za mashabiki hao kumhofia. Suarez ambaye anacheza katika klabu ya Liverpool alichukizwa na kitendo kilichoonyeshwa na mashabiki waliojitokeza katika Uwanja wa Millennium ambao walikuwa wakidhihaki wimbo wa taifa wa Uruguay ulipokuwa ukipigwa kabla ya kuanza kwa mchezo baina ya timu hizo. Suarez amesema kuwa mashabiki kumdhihaki na kumzomea yeye hilo halikuwa tatizo kwake lakini kitendo kilichoonyeshwa na mashabiki hao wakati wimbo wa taifa wa nchi yake hakikuwa kitendo cha uungwana na hakikupaswa kutokea. Mchezaji huyo amekuwa akizomewa mara kwa mara nchini Uingereza kutokana na tukio lake la kumtupia maneno ya kibaguzi beki wa klabu ya Manchester United Patrice Evra wakati timu hizo zilipokutana katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Uingereza ambapo alipewa adhabu ya kufungiwa michezo nane na faini kwa tukio hilo.
YANG AAMUA KUACHANA NA VINYOYA.
![]() |
| Yu Yang. |
MISRI, SENEGAL ZATINGA ROBO FAINALI OLIMPIKI.
WAWAKILISHI wa Afrika katika soka kwenye michuano ya Olimpiki inayoendelea jijini London timu za Misri na Senegal zimefanikiwa kusonga mbele katika michuano hiyo baada ya kutinga hatua ya robo fainali. Misri waliingia katika hatua baada ya kuichapa bila ya huruma timu ya Belarus kwa mabao 3-1 na kutinga hatua hiyo ambapo sasa watakutana na timu ya Japan katika mchezo utakaochezwa Juamosi katika Uwanja wa Old Traford jijini Manchester. Senegal nao walitinga hatua hiyo baada ya kutoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Umoja wa Falme za Kiarabu-UAE bao ambalo lilisawazishwa na mshambuliaji nyota wa timu hiyo Moussa Konate ambapo mpaka sasa amefunga mabao manne katika michuano hiyo. Nchi hiyo sasa itapambana na Mexico ambao wanaongoza kundi B baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Switzerland huku wenyeji wa michuano hiyo Uingereza wenyewe watacheza na Korea Kusini. Timu inayopewa nafasi kubwa ya kunyakuwa medali ya dhahabu kwa mara kwanza katika michuano hiyo Brazil wenyewe watamenyana na Honduras katika robo fainali ya michuano hiyo.
Wednesday, August 1, 2012
CARROLL AJUMUISHWA KIKOSI CHA LIVERPOOL.
![]() |
| Andy Carroll. |
VILLA KUREJEA UWANJANI KARIBUNI.
![]() |
| David Villa. |
SHEWEN ANYAKUWA DHAHABU NYINGINE.
![]() |
| Yen Shuwen. |
TAARIFA KUTOKA TFF: CHUJI, BAHANUZI WAITWA TAIFA STARS.
WACHEZAJI 21 WATEULIWA KIKOSI CHA TAIFA STARS
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen leo (Agosti 1 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 21 kwa ajili ya mechi ya kirafiki itakayochezwa ugenini Agosti 15 mwaka huu. Wachezaji walioitwa Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager wanatakiwa kuripoti kambi kwenye hoteli ya Tansoma, Dar es Salaam, Agosti 8 mwaka huu saa 1 jioni tayari kwa mazoezi yatakayoanza siku inayofuata. Makipa walioitwa kwenye kikosi hicho ni Deogratias Munishi (Azam), nahodha Juma Kaseja (Simba) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni nahodha msaidizi Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga) na Shomari Kapombe (Simba). Viungo ni Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Moshi (Simba), Mrisho Ngassa (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Ramadhan Chombo (Azam), Ramadhan Singano (Simba), Salum Abubakar (Azam) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar). Wachezaji wanaounda safu ya ushambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Said Bahanuzi (Yanga), Simon Msuva (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC).
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen leo (Agosti 1 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 21 kwa ajili ya mechi ya kirafiki itakayochezwa ugenini Agosti 15 mwaka huu. Wachezaji walioitwa Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager wanatakiwa kuripoti kambi kwenye hoteli ya Tansoma, Dar es Salaam, Agosti 8 mwaka huu saa 1 jioni tayari kwa mazoezi yatakayoanza siku inayofuata. Makipa walioitwa kwenye kikosi hicho ni Deogratias Munishi (Azam), nahodha Juma Kaseja (Simba) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni nahodha msaidizi Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga) na Shomari Kapombe (Simba). Viungo ni Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Moshi (Simba), Mrisho Ngassa (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Ramadhan Chombo (Azam), Ramadhan Singano (Simba), Salum Abubakar (Azam) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar). Wachezaji wanaounda safu ya ushambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Said Bahanuzi (Yanga), Simon Msuva (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC).
Subscribe to:
Posts (Atom)






