Sunday, October 2, 2011

ARSENAL YAENDELEA KUSUASUA, CHELSEA YANG'AA.

Add caption

LONDON, England
KATIKA Ligi Kuu ya Uingereza Arsenal imekubali kipigo cha nne katika ligi hiyo nyumbani kwa mahasimu wao Tottenham wakati mabao matatu ya Frank Lampard yaliisaidia timu yake ya Chelsea kuifunga Bolton katika mchezo uliochezwa Jumapili jioni.

Wachezaji Rafael van der Vaart na Kyle Walker ndio walioihakikishia Tottenham ushindi dhidi ya mahasimu wao Arsenal ambao iko mbili tu juu ya mstari wa kushuka daraja baada ya kucheza mechi saba.

Katika mchezo huo pia Arsene Wenger alipata pigo baada ya beki wake wa kushoto Bacary sagna kuumia mfupa wa ugoko, ambapo anatarajiwa kuwa nje ya dimba miezi mitatu.

Chelsea ni ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo baada lampard kuonyesha ubora wake katika Chelsea katika ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya timu inayoburuza mkia ya Bolton.

Matokeo mengine katika ligi hiyo kwenye michezo iliyochezwa jana ni kama ifuatavyo.

Bolton                1-5 Chelsea
Fulham   6-0 QPR
Swansea City 2-0 Stoke City
Tottenham 2-1 Arsenal

No comments:

Post a Comment