Saturday, October 29, 2011

KENYA KUCHAGUA VIONGOZI WAPYA WA SOKA.


UCHAGUZI wa uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu wa kuchagua viongozi wapya soka nchini Kenya unatarajiwa kufanyika leo baada ya kuahirishwa zaidi ya mara tatu.Wagombea nane wanatarajiwa kugombea nafasi za juu wakiwemo Mohammed Hattimy, Sam Nyamweya, Elizabeth Shako, Hussein Mohammed, Sammy Joel Obingo, Ambrose Rachier na Ally Twaha.Wagombea wamekuwa wakijinadi tofauti kwa wapiga kura wao ambapo Nyamweya amejinadi kuwa wakati alipokuwa kiongozi nchi ilikuwa katika nafasi za 68 na 70 katika viwango vya FIFA tofauti na ilivy hivi sasa.Hivi sasa nchi hiyo iko katika nafasi ya 135 katika viwango vya ubora vya FIFA.

No comments:

Post a Comment