Saturday, October 29, 2011

"ROONEY NI MSALITI KWA EVERTON." FERGUSON.

KOCHA wa Manchester United Sir Alex Feguson anaamini kuwa mshambuliaji wake Wayne Rooney siku zote bado anaonekana msaliti mbele ya mashabiki wa Everton ambao hawajamsamehe kwa kitendo chake kuihama klabu yake hiyo ya utotoni mwaka 2004.Akizungumza kabla ya mchezo wao wa leo dhidi ya timu hiyo katika Uwanja wa Goodison Park, Ferguson alisema mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza hawezi kusahaulika kwa kuikacha klabu hiyo kuelekea Old Traford kwa kitita cha paundi milioni 25 miaka saba iliyopita.Ferguson amesema hadhani kama wachezaji wa timu hiyo watamsumbua kwakuwa hakujawahi kutokea kitu kama hizo wakicheza na Everton huwa anaelewana nao vyema tu.Amesema tatizo liko kwa mashabiki kwakuwa huwa wanamuona ni msaliti na hilo haliweza kubadilika, na hilo huwa linajidhihirisha akifunga bao dhidi ya timu hiyo kwani mashabiki huwa wanamzomea.

No comments:

Post a Comment