Wednesday, November 16, 2011

AC MILAN YAMNYATIA DROGBA DIRISHA DOGO.

MAKAMU wa Rais wa AC Milan Adriano Galliani amesema angependa kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Didier Drogba katika dirisha dogo la usajili mwezi Januari mwakani. Timu hiyo vigogo nchini Italia hivi inakabiliwa na upungufu upande wa ushambuliaji baada ya mshambuliaji wake Antonio Cassano kuwa nje kwa miezi sita baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo. Galliani angependa pia kumsajili Nocolas Anelka au Mario Balotelli lakini akakiri kuwa Drogba ndiye chaguo lake la kwanza. Galliani amesema akiliambia gazeti moja nchini humo kuwa muda mrefu amekuwa akimpenda mshambualiaji huyo toka alipokuwa akicheza katika klabu ya Marseille ya nchini Ufaransa.

No comments:

Post a Comment