Monday, November 21, 2011

BECKHAM AISAIDIA GALAXY KUNYAKUWA KOMBE LA MLS.

TIMU ya Los Angeles Galaxy imefanikiwa kunyakuwa kombe la Ligi ya soka ya Marekani-MLS kwa kuifunga Houston Dynamo kwa bao 1-0 katika mchezo uliochezwa Jumapili usiku. Alikuwa ni nahodha wa Galax Landon Donovan ambaye alishinda bao hilo pekee dakika ya 72 akimalizia pasi murua ya Robbie Keane na kuihakikishia timu hiyo ubingwa wake wa kwanza toka waliposhinda mwaka 2005. Galaxy walionyesha dalili za ushindi tokea mwanzoni mwa mchezo baada kuonyesha kandanda safi karibu kipindi chote mchezo huo. Wakiwa na David Beckham ambaye alitua katika klabu hiyo mwaka 2007, Robbie Keane kutoka Ireland na Donovan katika kikosi hicho walikisaidia vyema kikosi hicho kuhakikisha kinashinda mchezo huo.

No comments:

Post a Comment