Monday, November 21, 2011

REDKNAPP FITI KUIVAA VILLA.

MENEJA wa Tottenham Hotspurs Harry Redknapp amesema anatarajia kuwa katika benchi la ufundi katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Aston Villa utakaochezwa leo katika Uwanja wa White Hart. Redknapp mwenye miaka 64 ambaye anatajwa Uingereza alikuwa nje katika baadhi ya mechi za ligi za ligi hiyo pamoja na ule wa ligi ya Ulaya dhidi ya Rubin Kazan baada ya kufanyiwa upasuaji mdogo wa moyo. Meneja huyo amesema kwasasa anajisikia vyema hivyo anaweza kuwemo katika benchi la ufundi la timu hiyo ambalo alimwachia msaidizi wake Joe Jordan na Kelvin Bond wamsaidie wakati yeye akijiuguza. Akihojiwa meneja huyo amesema alipata wakati mgumu kukitizama kikosi chake ambacho kiliifunga Fulham mabao 3-1 ni afadhali angekuwepo uwanjani.

No comments:

Post a Comment