Tuesday, November 22, 2011

MWAMUZI ALIYETAKA KUJIUA APATA NAFUU.

MWAMUZI ambaye alitaka kujiua masaa machache kabla ya kwenda kuchezesha mchezo wa Ligi Kuu nchini Ujerumani-Bundesliga mwishoni mwa wiki iliyopita ameruhusiwa kutoka hospitali. Shirikisho la Soka la nchi hiyo limesema katika tarifa yake Jumatatu kuwa mwamuzi huyo anayeitwa Babak Rafati ambaye ana umri wa miaka 41 hali yake inaendelea vizuri na anaendelea na matibabu. Rafati alikutwa alikutwa akitokwa na damu katika chumba cha hoteli alichofikia kabla ya mchezo wa Bundesliga kati ya Cologne na Mainz ambao alitakiwa kuuchezesha na sasa mchezo huo umeahirishwa mpaka Desemba 13 mwaka huu. Shirikisho hilo limesema kwasasa Rafati anahitaji amani na utulivu ambapo atahitaji muda na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu alichopitia.

No comments:

Post a Comment