Monday, November 28, 2011

PODOLSKI APATA AJALI.

MCHEZAJI wa kimataifa wa Ujerumani Lukas Podolski amepata ajali gari akiwa niani kuelekea mazoezini. Mchezaji huyo ambaye anakaribia kutimiza mchezo wa 100 toka aanze kuitumikia timu ya taifa aligongana na gari lingine lililokuwa na watu watatu wa familia moja. Watu wawili kati ya ya watatu waliokuwemo katika gari hilo walipelekwa hospitali kwa uchunguzi baada ya kupata majeraha madogo madogo. Podolski mwenye miaka 26 ambaye anakipiga katika klabu ya Cologne iliyopo katika ligi ya Bundesliga hakupata majeraha yoyote katika ajali hiyo ingawa chanzo cha ajali hakijajulikana mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment