Tuesday, December 6, 2011

CECAFA CHALLENGE CUP: KILI STARS YATINGA NUSU FAINALI.

TIMU taifa ya Tanzania Bara-Kilimanjaro Stars imetinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Challenge baada ya kuifunga Malawi kwa bao 1-0 katika mchezo wa robo fainali uliofanyika katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Bao pekee katika mchezo huo lilifungwa na kiungo wa Kilimanjaro Nurdin Bakari katika ya 16 ya mchezo ambapo sasa timu hiyo itapambana na Uganda ambao wameshinda kombe hilo mara 11 siku ya Alhamisi.

No comments:

Post a Comment