Wednesday, December 7, 2011

SPEED KUZIKWA WIKI HII.

Chama cha Makocha nchini Uingereza-LMA kumetoa taarifa kuwa mazishi ya aliyekuwa kocha wa timu ya Taifa ya Wales yatafanyika wiki hii. Katika taarifa yake hiyo chama hicho kilifafanua kuwa mazishi ya kocha huyo yatakuwa ni ya kifamilia, marafiki wa karibu na familia hiyo pamoja na wageni maalumu ambao watapewa mwaliko. Speed alikutwa amejinyonga nyumbani kwake Novemba 27 mwaka huu ambapo uchunguzi dhidi ya kifo chake kusogezwa mbele mpaka januari 30 mwakani. Taarifa ya LMA iliendelea kusema kuwa mjane na familia ya Speed ambaye pia aliwahi kuwa mchezaji akichezea timu za Leeds United, Newcastle na Everton inashukuru wote wakiwemo mashabiki wake walioguswa na kifo cha mchezaji huyo.

No comments:

Post a Comment