Wednesday, December 7, 2011

MILAN YAAFIKIANA NA TEVEZ.

KLABU ya AC Milan imefikia makubaliano ya kumchukua kwa mkopo mshambuliaji wa Manchester City Carlos Tevez. Ofisa Mkuu wa klabu hiyo Adriano Galliani amesema City wameonyesha nia ya kumuuza mshambuliaji huyo moja kwa moja kutokana na maelewano mabovu aliyonayo na kocha Roberto Mancini wao wako tayari kumchukua kwanza kwa mkopo. Gilliani amesema kwasasa wanamhitaji kwa mkopo kutokana na kutokuwa na uwezo wa kumlipa mshahara mkubwa kama anaolipwa na City hivyo ni matumaini yao wanaweza kumshawishi huko mbeleni kupunguza kiwango hicho ili wamchukue moja kwa moja. Milan wanasaka mshambuliaji kwa udi na uvumba katika kipindi cha dirisha dogo la usajili baada ya mshambuliaji wake Antonio Cassano kuwa nje kwa miezi kadhaa kufuatia upasuaji wa moyo aliofanyiwa.

No comments:

Post a Comment