Thursday, December 8, 2011

CECAFA CHALLENGE CUP: KILI STARS YAVULIWA UBINGWA.

TIMU ya taifa ya Uganda-The Cranes imetinga katika hatua ya fainali baada ya kuifunga Kilimanjaro Stars mabao 3-1 katika mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mabao yaliyofungwa na nahodha wa Cranes Andrew Mwesigwa, Emmanuel Okwi pamoja na moja la penati yalitosha kabisa kuizamisha Stars na kufuta ndoto zao za kutetea ubingwa huo. Bao la kufutia machozi la Stars lilifungwa na Mrisho Ngassa katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo. Kwa matokeo hayo sasa Uganda itapambana na Rwanda ambao katika mchezo wao waliocheza mapema leo walifanikiwa kuifunga Sudan bao 1-0 na kuingia fainali huku Stars wao wakicheza na Sudan katika mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu siku ya Jumamosi.

No comments:

Post a Comment