Friday, December 16, 2011

DONOVAN KUREJEA EVERTON JANUARI.

Timu ya Everton imefikia makubaliano ya kumchukua kwa mkopo mshambuliaji wa Los Angeles Galaxy London Donovan na kumrudisha tena Goodison Park mkopo ambao utakuwa wa muda mfupi. Meneja wa Everton David Moyes amesema amefurahishwa kuweza kumpata mchezaji huyo kwani atawasaidia katika kipindi cha mwezi Januari na Februari mwakani kwani alifanya vizuri wakati alipoichezea timu hiyo miaka miwili iliyopita. Donovan anatarajiwa kuwemo katika kikosi cha Everton kitakachoivaa Bolton katika mchezo wa ligi utakaochezwa Januari 4 mwakani ambapo mkataba wake unatarajiwa kuisha baada ya mchezo wa baina ya timu hiyo na mahasimu wao Liverpool Februari 25. Akihojiwa na tovuti ya klabu hiyo Donovan mwenye umri wa miaka 29 amesema ni nafasi ya kipekee kwake kurudi tena na kuichezea klabu hiyo inayoheshimika na yenye meneja ambaye amenisaidia kwa namna moja au nyingine kunifanya niwe mchezaji niliyekamilika.

No comments:

Post a Comment