Wednesday, December 7, 2011

GABON YAFUZU KUCHEZA OLIMPIKI.

Timu ya Taifa ya Gabon kwa mara kwanza imefanikiwa kufuzu kucheza michuano ya Olimpiki kwa mara ya kwanza baada ya kuifunga Senegal bao 1-0 katika mchezo wa vijana chini ya miaka 23 uliofanyika jijini Marakech, Morocco. Shujaa katika mchezo mchezo huo alikuwa ni mchezaji Andre Biyogo Poko baada ya kuunganisha kwa mpira wa kona dakika za mwisho za muda wa nyongeza baada ya timu hizo kwenda suluhu katika muda wa kawaida. Senegal itakuwa na nafasi nyingine ya kufuzu michuano hiyo itrayofanyika jijini London mwakani itakapocheza na hatua ya mtoano Jumamosi wakati katika mchezo mwingine wa nusu fainali utakaochezwa leo Misri itacheza na mwenyeji wa mashindano hayo Morocco. Timu tatu kati ya nne zilizoingia hatua ya nusu fainali ndizo zitakazopata nafasi ya kufuzu kucheza michuano hiyo ambapo timu itakayokamata nafasi ya tatu itabidi icheze hatua ya mtoano na kutoka bara la Asia mwakani.

No comments:

Post a Comment