Thursday, January 19, 2012

BECKHAM ASAINI MKTABA WA MIAKA MIWILI GALAXY.

Nahodha wa zamani wa Uingereza David Beckham anatarajiwa kurejea katika klabu ya Los Angeles Galaxy ya Marekani kwa mkataba mwingine wa miaka miwili. Katika taarifa yake Beckham amesema kuwa yalikuwa ni mamuzi muhimu kwake kwani klabu nyingi kutoka pembe zote za dunia zilikuwa zikimuhitaji lakini bado anafurahia kucheza soka nchini Marekani na kushinda vikombe akiwa na Galaxy. Beckham alindelea kusema kuwa ameshuhudia kwa mara ya kwanza mchezo wa soka unavyojizolea umaarufu nchini humo na ameamua kujikita zaidi kuukuza zaidi mchezo huo ambapo pia familia yake imeonekana kufurahia maisha nchini humo. Mkataba wa miaka mitano na Galaxy ulimalizika mwaka uliopita na kuna tetesi zilivuma kuwa Beckham ambye aliwahi kuzichezea klabu za Manchester United na Real Madrid alikuwa akitakiwa na klabu ya Paris Saint-German na baadhi ya vilabu vya Uingereza.

No comments:

Post a Comment